Sep 3, 2016

iPhone 7 to hit the market 

Wapenzi wa simu za mkononi hasa zinazotengenezwa na Kampuni ya Apple wanafahamu kuwa Septemba 6 mwaka huu historia nyingine itatengenezwa.
Siku hii inatarajiwa kuwa kampuni hiyo itazindua simu mpya aina ya iPhone 7, iPhone Plus na saa za Apple Watch 2.
Tetesi zilikuwepo kuwa kampuni hiyo inaandaa shughuli kubwa itakayofanyika Jumatano ya kwanza ya Septemba  katika Jiji la San Fransisco.
Ingawa simu hizo zinatarajiwa kuzinduliwa Septemba 7, inaelezwa kuwa zitakuwa madukani katika nchi zote kuanzia Septemba 16 mpaka 23.
Tetesi zinaeleza kuwa simu hiyo itakuwa kama ifuatavyo
·         Upana wa inchi 4.7 na urefu wa inchi 5.5 na hii ni kwa simu zote yaani iPhone 7 na iPhone 7 Plus.
·         Mwonekano wake hautakuwa tofauti na simu za iPhone 6 lakini inaelezwa kuwa haitakuwa na button ya kuanzia (home button)
·         Simu hizi zitakuwa na kamera kubwa iliyoongezwa uwezo wa kutoa picha nzuri.
·         Tetesi nyingine zinasema simu hizi hazitakuwa na tundu la kuwekea headphones na kwamba itatumia zile zisizo na waya.
·         Button ya kuanzia itakuwa ya kupapasa (touch screen)
·         Itakuwa na uwezo wa kuhifadhi kumbukumbu kati ya GB32 na GB256
·         Itakuwa na kasi ya A10 processor.
·         Itaendeshwa kwa mfumo iOS 10 
·         Itakuwa na uwezo wa kuzuia maji kuingia (water resistance)
·         Spika za kusikilizia muziki na sauti zimeboreshwa zaidi


No comments:

I have learnt that caring  too much on how your message will be conveyed unaweza kujikuta unabaki bubu. I’m a victim, you too at some poi...