Jun 18, 2016

Avic Town: My Dar es Salaam, My New Tanzania

The entrance

Kama ingetokea watu wakakubeba ukiwa usingizini na kukuacha katika eneo hili, hakika utakapoamka utasema “nataka niendelee kuishi hapa”, au labda ungeweza kusema: “Sirudi tena Tanzania, nitaendelea kuishi nchi hii,”.
Lakini hapa siyo Johannesburg, Afrika Kusini wala siyo Algiers, Algeria. Hapa ni Kigamboni jijini Dar es Salaam. Ni mwendo wa Kilomita 25 tu kutoka katikati ya Jiji la Dar es Salaam.
Inawezekana umeshawahi kuwa na ndoto ya kuishi mahali utakapojivunia kupaita nyumbani, eneo unalotamani kuona watoto wako wakikua kwa amani, sehemu itakayokuondolea msongo wa mawazo. Hapa ndiyo sehemu ya kupata mwafaka wa matamanio yako.
Moja ya mabango katika eneo hilo limeandikwa A place that gives you a peace of mind likimaanisha eneo ambalo linakupa tulizo la moyo wako. Kama unaishi hapa hakika utatulia lakini kama ni mpita njia utapata wakati mgumu kuaga.
Unapoingia katika eneo hili unakutana na barabara safi ya lami. Kutokana na mji ulivyojengwa. Kulia kwa geti hili kuna viwanja viwili vya michezo. Kipo kiwanja cha mpira wa miguu na kikapu.
Mbele zinaonekana nyumba zilizopangwa kwa ustadi wa hali ya juu. Siyo aina ya nyumba ambazo zipo katika miji yetu-mijini au vijijini.
Kutokana na hali halisi hasa za kiusalama, nyumba nyingi mijini zimezungushiwa kuta kubwa kila moja ikiwa na rangi yake hali ambayo hifanya mitaa kuonekana michafu.
Nyumba hizi zimetenganishwa kwa fensi ya nyaya inayowezesha upepo kupenya vyema. Upepo unapenya vyema na kuitofautisha hali ya hewa na maeneo mengi ya jijini la Dar es Salaam.
Mitaa yake haina mchanga lakini imesheheni kijani kibichi. Majani yameoteshwa kwa ustadi wa hali ya juu na kujengewa kwa vitofali  pembeni kwa utaalamu hali inayoyafanya mazingira yake yavutie kuyatazama wakati wote.
Maua na miti iliyooteshwa kwa mpangilio inalifanya eneo hili kuwa na harufu nzuri. Kila unapogeuka kuna mandhari nzuri ya kuvutia kutazama kutokana na ardhi hiyo kufunikwa na majani yaliyopangiliwa vizuri na kulifanya eneo ambalo halijafunikwa kwa lami au vitofali.


Such a nice place.....drooling





Avic Town ni nini?
Huu ni mji ambao jamii kubwa inaunganishwa katika viunga vya eneo lililopo Kigamboni jijini Dar es Salaam pembezoni mwa fukwe za amani.
Katika awamu ya kwanza nyumba zaidi ya 102 zimekwisha jengwa na zinauzwa kwa Watanzania tu.  
Msimamizi wa mauzo katika kijiji hicho, Lucy Makusa anasema nyumba hizo hazitauzwa kwa mgeni labda awe ameoa au ameolewa na Mtanzania.
“Hizi nyumba zinauzwa kwa Watanzania kwa sababu tunauza na ardhi, mgeni hawezi kununua nyumba hapa,” anasema Makusa.
Makazi hayawezi kukamilika bila kuwa na maeneo ya kibiashara, eneo hili pia lina eneo kubwa la maduka ya kisasa yatakayouza bidhaa mbalimbali.
Hakuna kwenda tena Afrika Kusini
Kwa wasanii hasa wa muziki wa Kizazi Kipya iliwalazimu kusafiri mpaka nje ya nchi hasa Afrika Kusini ili kupata mandhari nzuri kwa ajili ya upigaji picha za video.
Uwepo wa eneo hili umeanza kuwaondolea adha ya wasanii nchini kwani sasa wanarekodi nyimbo zao hapa nchini huku zikiwa na mandhari kama ya zile zilizotengenezwa nje.
Msanii David Genzi (Young D), Zuwena Mohamed (Shilole), Raymond Shaban (Raymond) na Baraka Andrew (Baraka da Prince) ni baadhi ya wasanii ambao wameshaitumia fursa hiyo kwa kurekodi nyimbo zako katika kijiji hiki.
Kama unataka kusafiri kwa macho kutoka hapo ulipo, tazama nyimbo Nyang’anyang’a wa Shilole, Kwetu wa Raymond au Ujanja Ujanja wa Young D utaona mandhari ya maeneo hayo.
Makusa anasema wamekuwa wakitoa fursa kwa wasanii kurekodi nyimbo zao bila  kuwatoza gharama zozote wakiamini kuwa kwa kufanya hivyo wanawasaidia wasanii.
“Lakini pia tunataka kuwaonyesha Watanzania kuwa kuna sehemu ambayo wanaweza kujivunia kwa kuwa ipo katika ardhi yao,” anasema Makusa.



Zipo nyumba za aina ngapi
Makusa anasema nyumba zipo za ukubwa mbalimbali. Nyumba za kawaida za vyumba vinne zipo 10, za vyumba vitatu zipo 30, za vyumba viwili ambazo ujenzi wake bado unaendelea zitakuwa 15, nyumba za ghorofa moja ambazo zitakuwa na vyumba vinne na vitano zitakuwa 77.
Nyumba za vyumba vitatu zimejengwa katika eneo lenye ukubwa wa mita za mraba 500, za vyumba vinne mita za mraba 700 na zile ghorofa zimejengwa katika eneo la ukubwa wa mita za mraba 1,000-1,500.

Ndani ya nyumba hizi
Nyumba kubwa ni za ghorofa moja zenye vyumba sita vya kulala. Hii imepewa jina la Premium Villa.  Mbali na vyumba vya kulala ina sebule mbili, chumba cha kuhifadhia nguo,  chumba cha kulia  chakula, majiko mawili na mabafu sita.
Aina nyingine pia ni ya nyumba za ghorofa moja waliyooiita Family Villa ina vyumba vitano vya kulala,  sebule mbili, chumba maalumu cha kuhifadhia nguo, mabafu manne na jiko la kisasa.
Nyumba za vyumba vitatu ambazo zinatoshea familia nyingi za Kitanzania zina chumba kikubwa cha kulia cha chakula, sebule kubwa, mabafu viwili na jiko moja kubwa.



The interior  is to crave for


Totauti na maeneo mengine
Wakazi wake kila mmoja atakuwa na kadi maalumu ya kuingilia ambayo atakuwa akiisugua katika mashine na geti litafunguka. Pia eneo hilo litalindwa saa 24 kwa mitambo ya kisasa.
Ni eneo ambalo mtoto anaweza kukua bila kujua adha ya kukatika kwa umeme na maji kama ilivyo kwa maeneo yote nchini.
Makusa anasema mazingira safi yanayoonekana sasa ndivyo yatakavyokuwa miaka 20 baadaye kutokana na mikakati iliyowekwa ya kuhakikisha maua, majani na miti vinatunzwa vilivyo.
Ujenzi unaendelea
Unapofika katika eneo hilo utaona ujenzi unaendelea, moja kati ya majengo yanayoonyesha kuwa katika hatua za mwisho mwisho ni jengo la kusambazia maji (water tower), bwawa la kuogelea na jengo la kufanyia mazoezi.
Ujenzi katika eneo hilo utaendelea baada ya awamu hii ya kwanza kukamilika.
Makusa anasema hiki kilichofanyika mpaka sasa ni sawa na robo tu ya mradi mzima.
“Uwekezaji wa hapa ni  ekari 583 lakini hapa ulipopaona ni ekari 44 tu, unaweza kutabiri ni jinsi gani hapa patakavyokuwa miaka mitano baadaye.” Anasema Makusa.

Kampuni inayoendeleza makazi haya
Kijiji cha Avic kinaendelezwa na Kampuni ya Avic Coast Land Development  iliyo chini ya Avic International ya nchini China.
Kampuni ya Avic International ni mashuhuri ulimwenguni kote  kwa biashara za usafiri wa anga, uchukuzi, uendelezaji wa makazi, usimamizi wa hoteli, uuzaji wa vifaa vya umeme na huduma za teknolojia.


ADIOS.

No comments:

I have learnt that caring  too much on how your message will be conveyed unaweza kujikuta unabaki bubu. I’m a victim, you too at some poi...